Mazuzu wawili walikuwa na uhusiano wa kimapenzi kwa muda mrefu sana; zuzu la kike na la kiume. Baada ya purukushani za hapa na pale, uhusiano wao ukavunjika. Yule zuzu dume hakuridhia na akaanza kumsumbua sana zuzu jike kwa kumpigia simu na kumtumia jumbe fupi za simu kila mara na kwa bahati mbaya zuzu jike alikuwa hapendi huo usumbufu.
Alitumia njia zote za kumzuia ikashindikana, ikabidi yule zuzu jike abadili kadi ya simu. Alipoweka ile kadi mpya tu, yule zuzu jike akatuma ujumbe mfupi kwa zuzu dume,
“Nimebadilisha namba, hutonipata tena mwanaharamu wewe!”
Yule zuzu dume alivyopata ule ujumbe akajibu,
“Nitahakikisha naitafuta hiyo namba yako mpya mpaka naipata!”
**********




