Home Masikani Je, Kuna Haja Ya Tanzania Kutoa Majeshi Yake Kulinda Amani?

Je, Kuna Haja Ya Tanzania Kutoa Majeshi Yake Kulinda Amani?

326
0

Darfur 1

Hawa ni baadhi ya askari wa Tanzania walijeruhiwa Darfur wakipata matibabu.

Kuna wakati unaweza ukajiuliza maswali, hivi ni kweli Tanzania tuhahitaji kuendelea kupigana vita ya nchi ambazo zimeshindwa kujitawala? Kwa manufaa ya nani? Na kwa nini nchi hizi zinaendelea kukosa utulivu? Inatuathiri nini iwapo tukaziacha nchi hizi? Je, kipato chetu kinatosha kushiriki vita za wenyewe kwa wenyewe?

Maswali haya na menngine mengi ni muhimu kujiuliza kwa sababu ya swali moja la msingi, ni nani anayefadhili makundi ya kiasi Afrika kwa kuyapa pesa na silaha? Hili swali ni muhimu kwa sababu mwisho wa siku sisi ndio tunaambiwa tukalinde amani katika nchi zenye waasi ambao hatujui ni nani anawafadhili. Kwa maswali haya ni dhahiri kwamba huu ni mchezo mchafu na kuna mkono wa mtu nyuma ya pazia!

Kwa mfano leo hii CHADEMA  wawe waasi kuipindua serikali ya CCM kwa mabavu halafu wakutwe wana silaha nzito za kivita; swali kubwa litakuwa wamezitoa wapi? Wamenunulia fedha kutoka wapi? Na wanaingia vitani kwa manufaa ya nani? Haya ndiyo maswali magumu ambayo siku zote viongozi wetu hutoa majibu mepesi, “wanaenda kulinda amani!”

Si vibaya kwa jirani kukiungua uende ukasaidie kuzima moto lakini kama jirani atakuwa anachoma nyumba yake makusudi ili ukamsaidie kuzima moto kila mara itafikia wakati azime mwenyewe na na akishindwa na aungue! Wala hii sio roho mbaya wakati mwingine watu hujifunza kwa njia zilizo ngumu! Mfano mzuri ni Rwanda, sitayazungumzia sana yale yaliyotokea Rwanda kwa sababu wengi mnayajua!


Hakikana nasema hakuna haja ya Tanzania kuendelea kupigana kwa ajili ya mataifa yaliyoshindwa kukaa pamoja kwa sababu kuu zifuatazo:-

  1. Hakuna asiyejua kama Tanzania imepigani nchi nyingi za Kiafrika zijipatie uhuru, kama ni mchango tumeshautoa sana kama Watanzania.
  2. je, ni kweli migogoro hii inayotokea katika nchi mbalimballi hususani Afrika imekosa utatuzi? Sidhani ninaamini kuna watu wapo kutengeneza migogoro kwa maslahi yao wanayoyajua wao, naamini watu wakipigana wengine watauza silaha!
  3. Mataifa makubwa yaliyoendelea kiuchumi ndio chachu ya migogoro mingi Afrika, hivyo kama ni kulinda amani mataifa hayo yatoe watu wake.
  4. Uchumi wa nchi yetu bado ni mdogo kutufanya kutumia jeshi katika vita isiyotuhusu, mtakumbuka vita ya Uganda ilivyotutia umasikini. Kupigana vita ni gharama kubwa sana ambayo hatuiwezi.
  5. Kumekuwa na uhalalishwaji wa wanaoitwa waasi kukubalika na mataifa makubwa, mfano mzuri ni Libya hivyo ni dhahiri kwamba watu wanapotoka kwenye mstari wa kiutawala kuna mataifa yanawaunga mkono na yawe ya kwanza kulinda amani.

Inawezekana kukawa na sababu nyingi zaidi za kuifanya Tanzania isishiriki katika vita hizi na zikatosheleza kurasa kadhaa za magazeti lakini ukweli unabakia pale pale, tunapigana vita isiyo na tija. Mawazo yangu nayaweza kuwa ya kiwendawazimu lakini ndio suluhu, aidha kuwaacha wamalizane ipo siku watapata akili kama Rwanda, au majeshi ya amani yawakamate waasi huko waliko, au nchi zinazotengeneza silaha ziache kuuza silaha kwa waasi!

 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here