Home Vichekesho Sasa Hivi Hata Kusalimiana Ni Ngumu Sana!!!!

Sasa Hivi Hata Kusalimiana Ni Ngumu Sana!!!!

532
3

Inavyoonekana dunia inakimbia sana na hakika mambo si shwari. Jamaa mmoja maarufu kwa jina la Rafael mkazi wa Tandika aliamua kuwakumbuka marafiki zake kwa kuwatumia jumbe fupi za maandishi kupitia simu yake ya mkononi.

Si unajua tena siku hizi makampuni yote yana vifurushi vya sms zaidi ya 100!  Rafaeli akaamua kutengeneza ujumbe mmoja maridadi kwa ajili ya marafiki zake;

“Vipi Jembe? Kitambo sana mwana, hivi uko pande za wapi vile? Nakupa hi tu kamanda wangu kama vipi pamoja sana”

Ujumbe huo ulikuwa kwa marafiki zake wa kiume na akatengeneza ujumbe mwingine kwa ajili ya marafiki zake wa kike ambao pia alikuwa anawafahamu japo kwa muda mrefu alikuwa hajawasiliana nao.

“Vipi mrembo? Pande za wapi? Kitambo sana sijakusikia! Nakupa hi mimi Rafael Hapa”

Baada ya kuziandaa jumbe hizo mbili tofauti aliamua kuzituma kwa marafiki zake watano wa kike na watano wa kiume. Baada ya dakika kadhaa Rafaeli alianza kupokea majibu ya jumbe zake!


Majibu ya marafiki wa kiume:

“Pamoja sana mwana, nipo town! Sikia mwana niko vibaya rekebisha hata buku 5 niione siku ya leo”

“Nipo mwana maisha tight, kama vipi nitoe jero ya vocha, choka mbaya hapa”

“Poa mwana niko busy, nitakucheki baadae! Sikia una msimbazi ya karibu hapo? Nitakucheck baadae nirushie kwa tigopesa plse!”

“Poa mwana, nina dili na wazungu fulani hivi ila nimekosa kianzio kama vipi niazime elfu 50, nitakurejeshea next week!”

“Mwana nimepatwa na majanga, nitoe 20,000/= nitakuelezea baadae yaliyonisibu!”

Majibu ya Marafiki wa Kike:

“Nipo poa, Rafael gani vile? By the way simu yangu imeisha credit nirushie 500 nijiunge tuchat!”

“Oh! Rafael, nipo saluni my dear nimepungukiwa elfu 10 naomba unirushie sasa hivi my dear!”

“Nipo Baby, nikwambie kitu Rafael bando yangu ya internet imeisha, naomba unirushie elfu 30 nijiunge plse Iam getting bored without Internet.”

“Nipo my dear maisha magumu, sana niwezeshe bosi wangu!”

“Nipo Rafael, birthday yangu jumapili utanipa zawadi gani?”

Baada ya kusoma jumbe zote hizo Rafael akajisemea moyoni, “Duh! sasa hivi itakuwa ni ngumu sana hata kumtumia mtu salamu!”

**********






3 COMMENTS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here