Home Makala Tanzania Si Nchi Masikini!

Tanzania Si Nchi Masikini!

442
0

Tanzania imekuwa ikitajwa kama moja ya nchi masikini zaidi duniani kwa miaka kadhaa sasa. Lakini upepo naona umebadilika kwani takwimu za hivi karibuni zinaonyesha Tanzania haipo katika orodha ya nchi 25 masikini zaidi duniani. Majirani zetu Uganda, Madagascar na Malawi wapo kweny nchi hizi masikini zaidi duniani.

Aidha kuna mengi ya kujihoji, ni kweli Tanzania si nchi masikini iwapo utathamanisha utajiri uliopo katika eneo la nchi hii. Pengine hiki ni moja ya vigezo vinavyoikwamua Tanzania na kuiondoa katika kundi hili. Ugunduzi wa gesi, chuma na madini ya Urani ni uthibitisho tosha kwamba Tanzania nia tajiri. Lakini tatizo kubwa ni namna Watanzania wengi wanavyoishi maisha duni licha ya utajiri huu.


Wageni wamekuwa wakifaidi na kuvuna utajiri wa nchi hii aidha kwa upumbavu au ulevi wa madaraka wa viongozi wetu waliopewa dhamana ya kutuongoza au uelewa finyu wa Watanzania juu ya kuzalisha mali kutumia maliasili walizonazo. Hii ni changamoto kubwa kwa Taifa hili linalotajwa kutokuwa masikini. Inakadiriwa miaka 10 – 20 ijayo Tanzania itakuwa nchi yenye uchumi wa kati!

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here