Mama mmoja alikuwa anapika chakula sebuleni si unajua tena nyumba zetu za kupanga hizi sebule na jiko na chumba cha kulala vipo sehemu moja; na ghafla akasikia mgeni anabisha hodi. Ikabidi afiche sufuria la chakula uvunguni mwa kochi. Baada ya kusalimiana mazungumuzo yao yalikuwa hivi,
Mgeni: Huo moshi ni wa nini?
Mama: Utaiweza mipanya ya humu kwa kuvuta bangi!
Mgeni: Na mimi naanza kuvuta bangi, bangi wanayovuta panya wako ina harufu nzuri sana, kama pialu!



