Mtanzania na Mkenya walienda super market kuangalia kama wanaweza kununua vitu. Baada ya kutoka Mkenya akawa anajigamba kwamba Wakenya ni wajanja sana kuliko Watanzania huku akimwonyesha Chokoleti tatu alizoziiba ndani ya super market.
Mtanzania akamshawishi Mkenya ili warudi tena ndani na yeye akamwonyeshe ujanja wake. Walipofika ndani Mtanzania akamwambia mhudumu;
Mtanzania: Nataka leo nikuonyeshe mazingaombwe
Mhudumu: Mazingaombwe gani hayo?
Mtanzania: Nipe Chokoleti tatu (Baada ya kupewa Yule Mtanzania akazila zote mbele ya mhudumu kisha akasema,) Unaona nimezila zote tatu lakini amini usiamini, chokoleti zako zote ziko mfukoni mwa huyu jamaa! (Anamwonyesha Mkenya)
Mhudumu akamkagua Mkenya na kweli akazikuta zile chokoleti tatu mfukoni mwake. Nani mjanja hapa?
**********




Ah mbavu ata hazijaexpand.
walipofika mtanzania akasema kwa mlinzi kuwa yule mkenya aliiba chocoldte kule ndani…haya sema nani mjanja hapo
Mtz mjanja banha
kweli nyie vunja mbavu nimewakubali.
mjanja mtanzania
Comments are closed.