Home Jamii Hakuna Ishara Ya VVU Kurudi Katika Ute Wa Mifupa Ya Wagonjwa Wawili...

Hakuna Ishara Ya VVU Kurudi Katika Ute Wa Mifupa Ya Wagonjwa Wawili Iliyopandikizwa, Wmesema Wanasayansi

395
0

Watu wawili ambao walikuwa na maambukizi ya VVU kwa muda mrefu wamesitisha kutumia dawa ya Ukimwi na hawana VVU  katika damu yao. Hii ni kutokana na matabibu kuwapa tiba ya kupandikiza uhondo wa mifupa katika mifupa yao na matokeo yameonyesha hakuna dalili za VVU kurejea katika mifupa yao.

“Kuhusu kinga ya UKIMWI, hatuwezi kulizungumuzia hilo kwa sasa, wallisema matabibu waliopo kwenye mkutano wa kimataifa wa Ukimwi huko Kuala Lumpur. “Ila huu ni mwanga mzuri katika kupata ufumbuzi wa tiba ya UKIMWI”, waliongeza matabibu hao.


Aidha majaribio haya yamewafanya waathirika hao wa VVU waache kabisa kutumia madawa ya Ukimwi. “Mmoja aliacha kutumia dawa miezi minne iliyopita na mwingine wiki saba zilizopita, hii haimaanishi Ukimwi umekingwa kwao”, aliongezaTimothy Henrich. Mgonjwa mmoja aliambukizwa miaka ya Ukimwi ulipoingia na mmoja aliambukizwa akiwa mtoto mchanga.

“VVU vinaweza kuwa sehemu yoyote ya ogani zao kama ubongo, ini nakadhalika, kama VVU havutarudi basi hata maeneo haya ni  mhimu sana kwa uhufadhi wa virusi na mbinu mbadala zitatakiwa kutumika kutambua uwezo wa VVU katika kujiunda”, aliongeza Timothy Henrich.

Maelezo Zaidi Kwa Kizungu

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here