Hongera kwa aliyepiga hii picha; ziara ya Obama nchini Tanzania ilivuta hisia za wengi duniani kote. Wapo aliohoji Obama kafata nini Tanzania? Wapo aliohoji pia kwa nini amekuwa akiiruka nchi ya Kenya kuitembelea pahala ambapo ni asili ya baba yake? Yote hayo ni maswali ambayo yalitawala katika ujio wake. Wapo waliotaka kumshika tu mkono na vinasa sauti na picha za video zilionyesha watu wakifurahia na kusema, “Nimemshika mkono”, hii yote ni kuonyesha shauku ya kumwona Obama waliyokuwa nayo watanzania wengi japo walibahatika wachache sana
Nampa tena hongera mpigaji wa picha hii ila mke wa mjomba alikosea, angepunga kwa mkono wa kushoto ingekuwa sare sare maua au mjomba angepunga kwa mkono wa kushoto ingekuwa kinyume na Obama na mkewe! Ni mawazo tu wala usiumize kichwa sanaaaaaaa!
