Shirika la afya dunian WHO limetoa ushauri wa kupunguza vifo vinavosababishwa na UKIMWI kwa kuwashauri waathirika waanze kutumia dawa mapema zaidi wakiwa bado wana kinga ya kutosha. Shirika hilo limesema, waathirika wa VVU wakianza kutumia dawa mapema itawasaidia kwa kiasi kikubwa kuwafanya waishi kwa muda mrefu zaidi kuliko wakisubiri kinga yao ikateremka sana.
Ushauri huo umetolewa Malesyia ambako kunafanyika mkutano wa kimataifa wa UKIMWI. Paul Ward, Mkurugenzi msaidizi wa Terrence Higgins Trust alisema, “hakuna sababu za kumfanya mtu afe kwa ajili ya UKIMWI!”

