Mwerevu na Mjinga walienda ktk usaili, walipofika kabla hawajaingia wakakubaliana aanze Mwerevu kisha akitoka ampe majibu Mjinga ili wote wapate kazi. Basi Mwerevu akaingia na maswali yakawa hivi:-
Msaili:- Tanzania ilipata Uhuru mwaka gani?
Mwerevu:- ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mpaka 1961 kutokana na sababu mbalimbali..
Msaili:- Nani hasa alihusika na upatikanaji wa Uhuru huo?
Mwelevu:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J.K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia.
Msaili:- Inasemekana ktk sayari ya Mars kunaviumbe wanaishi, je ni kweli?
Mwerevu:- Watu wengi wanasema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.
Baada ya Mwerevu kutoka basi Mjinga akapewa majibu yote..
Kuingia ktk usaili maswali yakawa hivi:-
Msaili:- Tuambie ulizaliwa mwka gani?
Mjinga:- Ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mbele mpaka mwaka 1961 kutokana na sababu mbali mbali.
Msaili:- Mungu Wangu, BABA yako anaitwa nani?
Mjinga:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J. K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia .
Msaili:- Hivi wewe ni chizi?
Mjinga:- watu wengi husema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.




