Home Vioja Wangapi Tutaingia Mji Ule? Jihoji Kama Nawe Utakuwemo!

Wangapi Tutaingia Mji Ule? Jihoji Kama Nawe Utakuwemo!

339
0

Mkasa huu ni wa kweli ulitokea nchini Rwanda wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe miaka ya 1990! Kipindi hicho kulikuwa na mapigano makali sana kati ya Wahtusi na Wahutu! Makabila haya yalichinjana sana kiasi cha kupelekea mauaji makubwa ya Kimbari ambapo inakadiliwa watu zaidi ya laki nane waliuawa!

Siku moja katika kanisa moja baadhi ya waumini wa kanisa fulani walikusanyika kwa ajili ya ibada. Siku hiyo yale makundi yenye ushawishi  yalikuwa yanataka watu wafanye kazi siku zote hivyo makundi hayo hayakuwa yanapenda kusikia watu hawafanyi kazi kwa kisingizio cha kusali na kadhalika.

cr image

Siku hiyo waumini wakiwa kanisani kundi moja lilivamia kanisa na kuwashurutisha watu watoke wakafanye kazi na si kusingizia kusali. Wote wakasema wamekuja ibada kwa ajili ya kuabudu! Kiongozi wa kundi hilo akasema wangapi wako tayari kufa kwa ajili ya Mungu wao? Bibi mmoja akawa wa kwanza kujitokeza na wengine wakamfuata huyo bibi wakapita mbele wakimaanisha wote wako tayari kufa kwa ajili ya Mungu wao.


Wale askari wakamchukua yule bibi wakazunguka naye nyuma ya kanisa na baada ya dakika kadhaa mmoja wa askari alikuja na jambia limelowa damu! Akauliza nani mwingine yuko tayari kufa kwa ajili ya Mungu wake? Wote wakakaa kimyaaaaaaa! Akauliza tena na tena alijitokeza babu mmoja na kijana mmoja wakapita mbele wakisema wako tayari kufa lakini wengine wakaogopa!

Baada ya tukio hilo yule bibi akaletwa akiwa hai na wale askari wakawaambia wale watu watatu yaani bibi, babu na yule kijana wao ndiyo watabaki kuendelea na ibada na siku zote wawe wanakuja kuabudu kila siku ya ibada na ikitokea wakawakuta wale wengine watawaua! Wakawapakia kwenye magari wakaenda kuwabaka na kuwachinja na wengine kuwafanya askari wao. Hakuna kumbukumbu zilizoandika mkasa huu japo ni kweli ulitokea!

Jumapili Njema!

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here