Kumekuwa na hulka na vijimambo fulani vya kiswahi-swahi ambavyo ni matukio ya kawaida tu lakini yamekuwa yakihusishwa na kupewa tafsiri za ajabu ajabu sana! Kwa mfano ikimruka mwenzako wanasema mwiko atakuwa mfupi! Ukilala umekunja miguu unaota unakimbizwa, mvua ikinyesha huku mvua inanyesha utaambiwa simba anazaa!
Kama simba kuzaa kila siku wanazaa maana ni kila siku wanapeana mimba kama wanadamu wanavyozaa na kupena mimba kila siku. Iweje leo hii mvua inyeshe huku jua lawaka useme simba anazaa!
Kuna jamaa mmoja alikuwa na viimani hivyo akawa anapenda sana kumwuliza rafiki yake kipenzi aliyekuwa anamwamini sana kila kinachomtokea ili ajue kina maana gani. Bila hiyana jamaa akawa anamjibu mwenzake kulingana na mahitaji yake.
Siku ya kwanza mazungumuzo yao yalikuwa hivi;
Jamaa: Nina washwa sana na viganya, hii ina maana gani?
Rafiki: Utapata pesa siku za hivi karibuni!
Jamaa: Nafumba macho nichore kiasi cha pesa kikubwa unachotaka nipate kwenye kiganja changu!
Kweli yule rafiki akaamchora kiasi cha milioni mia moja katika kiganja chake!
Siku nyingine tena jamaa akawashwa miguu ikabidi amwulize rafiki yake;
Jamaa: Ebwana swahiba leo nawashwa sana nyayo, maana yake nini?
Rafiki: Siku za hivi karibuni utapata safari!
Jamaa: Duh! Nitafurahi sana nikipata mchongo wa USA
Rafiki: Komaa tu mwana utafunga mkanda siku si nyingi!
Jamaa hakupata safari wala nini na maisha yakaendelea! Siku nyingine tena jamaa akapatwa na tukio ikabidi amwulize rafiki yake;
Jamaa: Swahiba kuna kitu kimenitokea sijui maana yake nini!
Rafiki: Kitu gani hicho?
Jamaa: Tangu jana nawashwa sana mkundu sijui maana yake nini!
Rafiki: Duh! Ebwana veri suni utakuwa msenge!
Ulizuka bonge la ugomvi!




kupata ela
Kupata ela 2
dalili ya Ukoma!