Jamaa mmoja siku chache zilizopita maeneo fulani ya jiji alikuwa anapenda kudowea futari iliyokuwa inaandaliwa na familia ya mzee mmoja maarufu sana hapa jijini Daslam! Mzee huyu maarufu amekuwa akiaanda futari kila siku jioni watu wanakuja kufuturu kwa raha zao si unajua tena mwezi wa mfungo huu!
Stori zikazagaaa kwamba kuna futari ya bure mitaa fulani hivyo hata wazamiaji wakaanza kuzamia ili kwenda kudowea futari la bure wakati wakijua wazi wao hawajafunga na futari hiyo ni mahususi kwa watu walio katika mfungo. Basi siku ya siku jamaa akajichanganya akazamia futari bila hiana. Watu wakakandamiza madikodiko muchuzi miksi, ikafika saa ya kushukuru na kutoa dua kwa ajili ya futuru. Bahati ikamwangukia yeye akachaguliwa kusoma dua. Huu hapa mkasa mzima , jamaa akaanza;
Mwenye nyumba: Naomba kijana utusomee dua.
Jamaa: (Huku macho yamemtoka akaanza)Ya Tawfiq
Watu: Amen
Jamaa:Ya Habibi
Watu:Amen
Jamaa:Ya Shabib
Watu:Amen
Jamaa:Ya Abood
Watu:Amen
Jamaa:Ya Hood
Watu:Amen
Jamaa:Ya Scandinavia
Watu: (Kimya)
Jamaa:Ya Ngorika
Watu: Mmmmmmmmmmmmmmmh!
Jamaa:Ya Dar Express
Watu: Jamani, huyu si anataja majina ya mabasi!
Wacha wamtoe nduki!
**********




Xaf sana
hyo nzuri alixahau Sumry
kazi nzuri,napenda sana.