Najua wengi wenu mnaoishi mjini mnafahamu nyakati za kulala zikifika kila mtu na siri zake kuhusu pale anapolaza mbavu zake ili kiza kipite. Wapo ambao hulala kwenye milango ya maduka ya watu, wapo wanaolala mitaroni, wapo wanaolala vichakani, wapo wanaolala kwenye magari mabovu, wapo wanaolala feri kwenye meli mbovu nakadhalika.
Lakini pia wapo wanaoanzisha urafiki na wenzao kila ikifika time ya kulala na kukipambazuka urafiki hakuna maana shida inakuwa imeisha. Ras mmoja alikuwa akipiga mishe zake kitaa ikifika saa ya kulala anaenda kuwaomba washikaji zake mbalimbali ili alale. Hivyo ilikuwa ndiyo desturi yake, leo atalala huku na kesho kule ili mradi siku zisogee.
Siku moja Ras huyo alichelewa kama kawaida yake akaamua kupita maeneo ya Sinza Kijiweni kwa mmoja wa rafiki zake ili ampe hifadhi kwa usiku huo. Baada ya kufika yule Ras aligonga mlango kama ishara ya kubisha hodi ili afunguliwe. Baada ya mazungumuzo ya awali Ras alieleza shida yake ni kulala kwa usiku huo mmoja tu. Yule jamaa mwenye gheto ikabidi amwulize jina na mazungumzo yao yalikuwa kama ifuatavyo,
Mwenye Gheto: We nani?
Ras: Rasta Farrai Jah Blessing King of Haile Sellasie Jah Man Gwan Man Bum Bum Peace and Love Forever Nigga!
Mwenye Gheto: Hapana sifungui, mpo wengi sana, Gheto langu dogo hamtaenea.
**********




??
H2H