Home Vichekesho Teja Na Mfungo Mtukufu

Teja Na Mfungo Mtukufu

391
0

Kuna kawaida ya kituo fulani cha luninga huwa kinafanya mahojiano ya watu mbalimbali katika mitaa na kuwapa fursa ya kutuma salamu kwa ndugu jamaa na marafiki. Mtangazaji wa kipindi hicho wakati akifanya harakati za kipindi chake siku chache zilizopita alijikuta anakutana na kundi la mateja maeneo fulani ya Daslam!

Bila kupepesa macho teja mmoja akausoma mchezo naye akaamua kumlazimisha mtangazaji amhoji. Baada ya kutafakari sana yule mtangazaji akaamua kukubali kumhoji yule teja na mazungumzo yao yalikuwa hivi,


Matangazaji: Unaitwa nani?

Teja: Maalim Jumaaaaaa!

Matangazaji: Unaishi wapi?

Teja: Hapa hapaaaaaa!

Mtangazaji: Tuma salamu basi kwa ndugu jamaa na marafiki!

Teja: Ahaaa! Nawapa hai masela wangu wa Manzese, majita wote wa Sinza Uzuri bila kuwasahau wana wangu wote wa Kawe Ukwamaniiiii!

Mtangazaji: Ujumbe?

Teja: Nimefungaaaa situmii doziii mpaka jua litueeeee! Majita wote waniigeeeeee!

Mtangazaji: Unachagua wimbo gani usindikize salamu zako?

Teja: Sitaki Wimbo! Nipigie ADHANA nikafuturu nina ubao balaaaaa!

**********

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here