Hapa wenye pesa wamechoka kusubiri!
Kama ni mchezo ambao unatakiwa upelekwe katika michuano ya Olympic ni pamoja na mchezo wa ‘kupeana pesa’ yaani kuweka na kukopa na wengine huuita upatu! Kina mama wengi wamekuwa wakishiriki michezo hii kwa kudunduliza kiasi kidogo cha pesa ili waweze kufanya mambo ya msingi.
Lakini pia ni kawaida ya watu wanaokuwa na dhamana kutafuna bila huruma pesa za watu na kuwawekea vizingiti vingi na kila namna ya mababaisho ili kupoteza haki zao! Hii sijui ni kutokana na usemi unaosema pesa ni mwanaharamu!
Katika mkasa huu utashuhudia kina mama nchini Kenya wakivurumusha matusi ya nguoni kwa mtu anayedhaniwa kumung’unya pesa zao na pia kuwatanga kimapenzi kabla ya kuwatimizia mahitaji yao! Nisiwe mwandikaji sana!

