Kumekuwako mikasa mingi ya ukatili ambayo imekuwa inafanywa na wazazi yaani kina mama kwa watoto wao. Kama hujawahi kushuhudia mtoto akitupwa chooni au jalalani basi umewahi kusikia au kusimuliwa. Visingizio vikubwa huwa ni ugumu wa maisha na kukimbiwa na wazazi wenza yaani wanaume ndiko kunakopelekea mabinti wengi kuua watoto wao!
Nasema mabinti kwa sababu naamini mwanamke aliyepevuka hawezi kutupa mtoto wala kumwua kwa kisingizio cha ukata japo kuwa wapo wanawake wanaofanya hivyo pia.
Lakini video hii inaripoti tukio la ajabu na la aina yake kidogo kwa mtoto ambaye ni mdogo sana anapigwa mpaka inatia huzuni kwani ni ngumu sana kuiangalia video hii. Huyu mama hakutakiwa kufanya hivi kwa sababu zifuatazo:
- Mtoto ni mdogo sana kiasi kwamba ukasema kafanya kosa la kuadhibiwa vile.
- Mpiga picha za video hii alikuwa anaweza kuacha kurekodi na kumzuia huyu mama asifanye hivyo.
- Kuna watu wengine kadhaa wanaonekana walikuwepo wangeweza kuzuia hilo pia lisitoke.
Lakini kwa bahati mbaya sana hayo yote hayakufanyika, hebu angalia video hii uhuzunishe moyo wako!

