Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ametolea ufafanuzi juu ya ujio wa Rais Obama Tanzania. Akiongea na vyombo vya habari kwa nyakati tofauti, Rais Kikwete ameeleza kuwa ni kweli Rais Obama alipanga kuja kwa muda mrefu sasa lakini kulikuwa na mambo ambayo yalikuwa yakikwamisha hiyo safari yake kukamilika. Jambo ambalo limeshtua ni kwamba Rais Kikwete hajui has aObama atakuja kufanya nini hivyo kama ilivyo kwa Watanzania, na yeye anasubiri hiyo ‘suprise’!
Rais Kikwete aliongeza kuwa, huu sasa ni wakati mwafaka kwa Rais Obama kuja Tanzania ndio maana taarifa zimekuwa wazi sasa kwa umma. Kipindi hiki ni kipindi ambacho kitakuwa na wageni wengi na Tanzania inatarajia pia ujio wa wakuu wa nchi mbalimbali wanaokuja kwenye mkutano wa wakuu wa nchi kujadili mambo ya maendeleo katika nchi zao.
Angalia video yake hapa
