Siku ya tatu mvua imekolea Daslam wenye michepuko yao wakaamua kutumia mwanya huo ili kufanya yao! Mkasa mzima ulikuwa hivi:
Mume: Halloo mke wangu.. yaani ni shidaa sitaweza kurudi nyumbani daraja limevunjika na kutoka morogoro kurudi Dar haiwezekani!
Mke: Mume wangu Morogoro ulienda bila kuniaga! ?
Mume: Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu sikuweza kukwambia!
Mke: Khaaa! Sasa watoto nani atawaangalia!!!
Mume: Unasemaje!??? Wewe uko wapi kwani???
Mke: Niko Bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi!
Mume: Unasemaje wewe mwanamke…???? Nakwambia hivi nikukute nyumbani ndani ya dakika 15!
Baada ya dakika 15 mume kafika nyumbani!!!!!!
Mke: Haya umefikaje kutoka Morogoro?
Mume: Nilipewa lift na helikopta ya Rais nilikuwa na makamu wake pia!!!!
Mke: Wewe mwanaume si helikopta aliyokuwemo makamu wa Rais imepata ajali kabla ya kuruka uwanja wa ndege wa Dar es salaam..
Mume: Mimi ni majeruhi mmojawapo!!!!




