Home Vichekesho Asili Ya Binadamu Ni Nini? Ushawahi Kuulizwa Swali Hilo Na Mwanao?

Asili Ya Binadamu Ni Nini? Ushawahi Kuulizwa Swali Hilo Na Mwanao?

641
1

Watoto ni wadadisi sana na kuna wakati usipokuwa makini ipo siku mwanao atakuja kukuona wewe kilaza! Kama hiyo haitoshi limekuwa ni jambo la kawaida kwa wazazi wengi wakiulizwa maswali makubwa makubwa na watoto wao hutafuta majibu ya uongo ili kuwaridhisha au kuwaepusha na kadhia hiyo ya maswali ambayo mara nyingi huwa ni magumu kuyajibu.

Siku moja mtoto mmoja alimwuliza baba yake;

Mtoto: Hivi baba, mtu wa kwanza kabisa duniani alitokea wapi?

Baba: Adam na Eva waliumbwa na wakazaa watoto, wale watoto nao wakazaa watoto mpaka dunia ikawa na watu wengi unaowaona.

Baada ya majibu hayo, yule mtoto alitaka kwenda kuhakiki kwa mama yake. Hivyo aliamua kumfata mama yake na kumwuliza swali ilo hilo;


Mtoto: Hivi mama, mtu wa kwanza kabisa duniani alitokea wapi?

Mama: Hapo mwanzo tulikuwa nyani, muda ulivyokuwa unaenda tukawa tunabadilika mpaka tukawa watu!

Yule mtoto akatoka mbio mpaka kwa baba yake na kumwambia;

Mtoto: Umenidanganya baba, mbona mama kasema mwanzo tulikuwa nyani?

Baba: Sijakudanganya mwanangu, hiyo ni asili ya familia ya mama yako!

**********




1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here