Hii Inawahusu Wazee Wa 49%
Jamaa akiwa nyumba ndogo karelax na Mdada, Mdada kwa sauti laini akaanza;
MDADA: Jamani lini utanyoa hizo ndevu, mi sizipendi
JAMAA: Bwana ziache mke wangu anazipenda sana hatutaelewana nikizinyoa!
MDADA: Nyoa jamani, au hunipendi?
JAMAA: Nakupenda, lakini kwa nini huzipendi?
MDADA: Unajua we handsome boy sana mpenzi, mi nataka niwe nauona uso wako wote swiry…
Jamaa hatimae akanyoa ndevu zote. Baadae akarudi nyumbani usiku akinyata taratibu na kufanikiwa kupanda kitandani akalala. Mke wake akiwa usingizini akageuka na kumgusa mashavu,
MKE: We James, huogopi kufa, mume wangu atarudi muda wowote, ondoka haraka bwana!




