
Mchungaji na mkewe mtarajiwa dakika chache kabla ya ndoa yao kuingia dosari.
Hili ni tukio la kusikitisha na kufedhehesha zaidi kuwahi kulisikia lakini lenye mafunzo kibao ndani yake. Tukio hilo lilitoke mwanzoni mwa mwezi wa nane mwaka huu ndani ya kanisa mojawapo la Pentekoste nchini Kenya ambapo wanandoa wawili walikuwa wakila kiapo cha maisha mbele ya mchungaji wa kanisa hilo. Jambo la kufedhehesha zaidi ni kwamba yule mwanaume aliyekuwa anaoa yaani bwana harusi na yeye ni mchungaji katika kanisa hilo.Hakika hii ni vunjambavu……….
Dakika chache kabla ya wanandoa hao kuapishwa na kuruhusiwa kuvishana pete, Mchungaji wa kanisa hilo aliwauliza waumini kama kuna yeyote mwenye pingamizi la kufungwa kwa ndoa ya wapenzi hao jambo ambalo hufanywa na wachungaji wengi kwa mujibu wa taratibu za ndoa za kikristo!
Baada ya swali hilo, mwanamke mmoja alisimama na kuelekea mbele ya kanisa hilo huku akiwa na vyeti mkononi. Alipomkaribia mchungaji, mwanamke huyo alipaaza sauti yake na kusema kuwa ndoa hiyo haistahili kufungwa kwa sababu yeye na bwana harusi wana mtoto waliyemzaa pamoja na kwamba walikuwa na mipango ya kuoana! Huo ndiyo ukwa mwanzo wa sakata hilo la kusisimua!
UNATAKA KUJUA KILICHOTOKEA BAADA YA HAPO?
ANGALIA VIDEO YAKE HII HAPA!!!!!!!!!!!!!!!!!!

