Kwa kweli kuwa mwalimu ni kazi sana na yakupasa ufikirie mara tano zaidi ya mwanafunzi kwa sababu wapo wanafunzi waliojaliwa uwezo mkubwa na wa kipekee kufikiri hivyo usipoangalia unaweza kujikuta unaaibika.
Mwalimu wa shule moja ya chekechea alikuwa anawafundisha watoto wake namna ya kujitambua na kupambanua mazuri na mabaya. Nia yake kubwa ilikuwa kutaka kuwafanya watoto wajue ni jambo gani sahihi na jambo gani si sahihi.
Wakati anaendelea na darasa, mwalimu huyo aliwauliza wale wanafunzi swali;
Mwalimu: Anayejiona yeye ni MPUMBAVU asimame juu!
Katika hali ya kushangaza mwanafunzi mmoja akasimama juu kwa kujiamini na wenzake wakaanza kumcheka. Mwalimu hakutaka kuonyesha papara akaamua kumhoji yule mtoto kwa nini kasimama, ina maana yeye ni mpumbavu;’
Mwalimu: Amin, kwa nini umesimama?
Amin: Sikutaka kukuacha uendelee kusimama peke yako!
**********




Bora msitoe story za namna hii story gan nusu
Noma dogo kamsaidia ticha asiwe pekeyake ametisha
ht mm kwny PC yangu naona story nusu na hamna sehemu ya kuxoma zaid. zaid naona k2n kwa chn 2! labda wanao2mia cmu?!