Kuna jamaa mmoja alihangaika sana kutafuta kazi. Siku moja alibahatika kuitwa katika usahili baada ya kuteuliwa kufanyiwa usahili. Kama unavyojua usahili mwingi hufanyika kwa lugha ya kizungu yaani kiingereza.
Yule jamaa alipofika eneo la usahili akapokelewa na mmoja wa mabosi waandamizi na msimamizi wa usahili; na mazungumuzo yao yalikuwa hivi;
Bosi: Good morning
Jamaa: Good morning sir
Bosi: Have you attended the interview?
Jamaa: Yes sir.
Bosi: Wait
Jamaa: 75 Kilogram sir!
Unachezea Kizungu wewe katika interview! Huwa kunazuka vituko ni balaa!
**********



