Ni kweli mawazo mengi sana yameshafanyiwa kazi na watu mbalimbali duniani hivyo ni vigumu sana kuja na wazo jipya kabisa. Hata vitabu vya kiimani vimeandika hakuna jipya chini ya jua.
Lakini jambo ambalo siwezi kulikubali sana ni copy and paste! Unaweza kuwa ni mtazamo wangu hasi lakini kukopi kunaondoa ladha ya kile kitu unachokidurufu!
Tumekuwa tukiona mara kadha wa kadha wasanii wetu wa kibongo wamekuwa wakibeba tuzo kwa umahiri wao wa kutunga nyimbo na midundo lakini wapo pia wanaobeba tuzo kwa migongo ya wengine. Angalia video hizi mbili, moja ni ya Ben pol wimbo waitwa Jikubali na video ya Wimbo unaitwa The Script wa Hall of fame
Bofya Hapo Chini Kuangalia Nyimbo Zote Mbili

