Wakati fulani ni vigumu kufahamu au kuhisi watu wanakuonaje. Inawezekana kabisa jinsi unavyojiona wewe sivyo watu wanavyokuona. Jamaa mmoja aliyefahamika kwa jina la Majuto aliamua kujitathimini na kutaka kujua rafiki zake wanamwona ni mtu wa namna gani.
Ili kufanikisha utafiti huo, Majuto aliamua kuwapigia simu marafiki zake watatu kwa nyakati tofauti tofauti. Majibu ya watu wawili wa mwanzo hayakumridhisha kabisa akadhan anaota na akaamua kujaribu kumsikia na mtu wa tatu atamwambiaje na mambo yalikuwa kama hivi,
Majuto: Hallo, Niambie Jembe?
Mashaka: Poa mwana uko njema?
Majuto: Niko njema mwana!
Mashaka: Mbona leo simu asubuhi asubuhi mwana, umekesha na ‘misukule’ nini?
Majuto: Ahaaa! Acha bana ! Majanga mwana, nipo Osterbay nimelala ndani!
Mashaka: Nini tena swahiba?
Majuto: Naomba nikuulize mwana, sasa hivi umesikia nimekamatwa, unafikiri naweza kuwekwa ndani kwa kosa gani?
Mashaka: Ubakaji!
Majuto akashusha puumzi na kuzimia! Jaribu na wewe uone marafiki zako wanakuchukuliaje!
*Misukule = Machangudoa ambao huingia kwenye gheto za watu saa tano usiku nakutoka saa 11 alfajiri ili majirani wasikuone kama ulilala na Changu!
**********



