Ni mara ngapi umewahi kuingia hotelini kununua chakula na baada ya kuchagua chakula kile unachokipenda basi ukaagiza na kuletewa. Lakini ukiwa katikati ya mlo ukaona mwenzako ameletewa chakula kingine na ukawaza kuwa ni bora ungenunua kile ambacho anakula mwenzako? Nafikiri imewahi kukutokea hivyo!
Mwanamume mmoja alimuomba Mungu amjalie ageuke kuwa mwanamke,kwa sababu alihisi mke wake anafaidi kubaki nyumbani wakati yeye anapiga kazi saa kumi mfululizo. Mungu hakuwa na hiyana,asubuhi alipoamka,akajikuta tayari amekuwa mwanamke. Haraka haraka akamtayarishia ‘mumewe’ chai ili aende kazini, akaogesha watoto, akawapa chai na kuwatayarisha kuwapeleka shule.
Wakati anarudi, akapitia sokoni kununua mahitaji ya siku. Kufika nyumbani,akaanza kusafisha nyumba na kufua nguo. Wakati anataka kutayarisha chakula, akagundua kuwa umeme umekatwa kwa sababu ya deni. Ikabidi atoke mbio kwenda kulipa bili ya umeme. Alipotoka kununua umeme wakati wa kwenda kuwachukua watoto ulishafika ikabidi apitie shule.
Kufika nyumbani akaanza kutayarisha chakula huku watoto wanamlilia njaa. Kwa ufupi, hadi kufika wakati wa kulala, bado hakuwa hajamaliza kazi zote, ikambidi aingie kitandani vivyo hivyo.
Kitandani nako hakukuwa na kupumzika.’Mume’ alitaka apewe kidogo, hakumkatalia. Lakini baada ya kumaliza tu akamuomba Mungu akisema,
“Mungu wangu,nimefanya makosa,kwani kazi anazo fanya mke wangu ni kubwa kuliko nilivyokuwa nikifikiria.Naomba unirejeshe katika hali yangu ya zamani.”
“Hakuna taabu kiumbe wangu”,
Mungu alimjibu na kuendelea,
“Ombi lako nimelikubali, lakini itabidi usubiri miezi tisa kwani jana ulipofanya mapenzi na mume wako,ulishika ujauzito!!”
**********




Nyce story add Mor than that.
Xna 2
Vunja mbavu