Sehemu pekee ambayo huuza bidhaa na kutoa sehemu ya matumizi ya bidhaa hiyo ni baa na kwenye mahoteli. Kwa hakika sehemu nyingine ‘tunafosi’ tu! Jamaa mmoja alienda kwenye duka la Mangi mmoja lililopo maeneo ya Kinondoni Studio Daslam kununua sigara! Baada ya kununua sigara zake jamaa akaomba kibiriti ili awashe sigara yake.
Alipoiwasha jamaa akaanza kuvuta na kuipuliza pale pale. Kitendo hicho kilimkera sana muuzaji katika duka lile na uzalendo ukamshinda akaamua kufunguka!
Muuza bidhaa: Samahani kaka hairuhusiwi kuvuta sigara hapa.
Mteja: Kheeeee!
Muuza bidhaa: Ndio hivyo bosi!
Mteja: Haya maajabu! Lakini sigara si nimenunua hapa hapa ndugu yangu? Unataka nikavutie wapi?
Muuza bidhaa: Mbona kila siku nakuuzia kondomu hautumii hapa hapa?
Mteja: Hujawahi kuniambia kama una gesti hausi hapa! Ningekuungisha na hela ya chumba!
**********




DAAA