Imeripotiwa kwamba Rais wa zamani wa Marekani Goerge Bush SR., alituma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii akitangaza kifo cha Nelson Mandela jumamosi ya wiki iliyoisha! Bush mwenye miaka 89 alituma salamu za rambirambi ambazo zilinaswa na mitandao ya habari ya Kimarekani na kurushwa CNN.
Jim McGrath, msemaji wa Bush alituma baruapepe yenye kichwa cha barua kisemacho, “Tamko la Rais Goerge H.W. Bush Kuhusiana Na Kifo Cha Nelson Mandela.” Aliandika kwa niaba ya Bush, “Mimi na Barbara tunaomboleza kifo cha mmoja wa wakereketwa wakubwa wa uhuru duniani ambao tumewahi kuwaona.”
“Nikiwa Rais, nilishuhudia jambo la kipekee la kuwasamehe watu waliomfunga kimakosa kwa miaka 26 gerezani na kuonyesha ukombozi wa kweli na ukarimu wa aina yake kwa kila mtu. Alikuwa mtu mwenye maadili na aliibadili kwa kiasi kikubwa historia ya nchi yake. Mimi na Barbara tunatoa heshima zetu zote kwa Nelson Mandela na tunatuma salamu za rambirambi kwa wanafamilia wote na wananchi wote wa Afrika ya Kusini.”
Lakini Mc Grath alijibu baadae kupitia mtandao wa Tweeter kwamba taarifa hiyo ya Bush ilitokana na taarifa za awali kutoka Washington. Aidha baadae Mc Grath aliongeza kwa kuomba msamaha baada ya kutoa tangazo ambalo halikuwa sahihi.
Taarifa za hivi karibuni zinaeleza kwamba Nelson Mandela ametolewa hospitali na kurudishwa nyumbani kwake Johannesburg siku ya jumapili asubuhi ambako anaendelea kuwa chini ya uangalizi wa matabibu. Mandela ana umri wa miaka 95 sasa.
Chanzo: The Telegraph

Du watu kupenda matatzo ya wengne
Bush angalia mzee usije ukaingia kikaangoni
He
Bush kulikoni?