Home Vichekesho Bikini Zamwumbua ‘Hausi Geli’ Na Bosi Wake!

Bikini Zamwumbua ‘Hausi Geli’ Na Bosi Wake!

618
3

Imekuwa ni kawaida kwa watu wengi kuajiri mabinti kwa ajili ya usaidizi wa kazi za ndani. Ili kudumisha nidhamu mara nyingi mabinti hao wanaofanya kazi za ndani maarufu kama ‘mabeki tatu’ huwa wanafunzwa kuwaita mabosi wao baba na mama!

Hii ilitokea maeneo fulani ya jiji la karaha na mikasa Dar es Salaam ambapo mama mmoja aliyekuwa ameolewa na kubahatika kupata watoto wawili alikuwa anaishi pia na huyu mfanyakazi wa kazi za ndani. Ikafika wakati yule mama akawa akianika bikini zake bafuni zikawa zinapotea katika mazingira ya utata kumbe kulikuwa na panya ambaye alikuwa anazibeba na kupanda nazo darini.


Moja kwa moja yule mama akawa anaamini kwamba binti yake wa kazi alikuwa anaziiba na mazungumuzo yao yalikuwa hivi,

Mama: Weee! Mdada hivi chupi zangu nani anazichukua huko bafuni kila nikianika?

Hausi geli: Mimi sijui mama!

Mama: Wanawake humu ndani tuko wawili tu nani mwingine aziibe?

Hausi geli: Kweli mama sijaziiba mimi, kama huamini mwulize hata baba kama mimi huwa navaa chupi zako!

**********

3 COMMENTS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here