Kumekuwepo namna moja au nyingine ya kutojivunia Kiswahili kitu kinachopelekea zoezi la kutumia lugha ya Kiswahili katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu, sheria na kwingineko kuwa ni kitendawili. Wanafunzi wamekuwa wakijifunza masomo ya Kiingereza katika nchi ya waswahili kwa lengo la kuelimika ili wawahudumie waswahili. Hali hii imepelekea kuwa na wahitimu ambao hawawezi kushindana kwa sababu ya kutokukifahamu vema wanachokisomea au kushindwa kukielezea.
Ifuatayo ni video ya wanafunzi wa Chuo kikuu cha Indiana (Bloomington Campus) wanaojifunza Kiswahili katika mambo ya habari na siasa wakijaribu kufanya mjadala wa kampeni za wagombea urais wa Tanzania Bi Amina na ‘Mbowe’! Inawezekana wanafahamu sana kinachotokea Tanzania na nisikuharibie utamu, ichukue hii hapa uangalie mwenyewe video yake.


So good