Mwanamke mmoja aliamua kujipima kwa mumewe ili ajue mume wake alimpendea kitu gani. Jambo hilo lilikuwa linamwumiza sana kichwa kwani hakuwahi kusikia hata siku moja mume wake akimsifia kwa chochote kuhusiana na umbile lake.
Lakini mwanaume huyo aliendelea kusisitiza kuwa anampenda sana mkewe. Jambo hilo lilimfanya mwanadada huyo kuvunja ukimya na kuamua kuhoji;
Mke: Hivi mume wangu naomba leo uniambie, ni kitu gani hasa kinakufanya unipende? Hivi ulinipendea nini my love? Au makalio yangu makubwa maana nina vichuguu! Au sura yangu iliyorembeka? Hebu niambie au jicho langu la kulegea!
Wakati wote huo mumewe alikuwa amekaa kimyaaaaa!
Mke: Hebu niambie basi my dia, au mwanya wangu!
Baada ya hapo yule mwanaume akamwangalia mke wake kutoka nywele mpaka kucha za miguuni kisha akajibu.
Mume: Kusema kweli mimi nakupendea kitu kimoja tu!
Mke: Kipi hicho! (Akadakia kwa haraka akitaka kujua) Au mwanya?
Mume: Ni kweli una mwanya tena sio mmoja, kwa haraka haraka naona kama una mianya kama kumi juu na chini! Na kwa bahati mbaya siipendi maana inafanya ulimi wako uonekane kama uko selo!
Mke: Mh! Yamekuwa hayo, sasa wanipendea nini?
Mume: Ukarimu wako na roho yako ya kibinadamu tu ndiyo vyanikosha!
Kwa kweli kilichotokea hapo hata sijui!
**********




Whatttttt…..slap ur husband…
haaah