Kuna jamaa alikaa muda mrefu sana bila kupata mtoto. Akiwa anakaribia kufikisha miaka 45, jamaa alibahatika kupata mtoto wa kiume! jambo hilo lilimpa furaha sana akawa anajisifu kwa watu! Siku moja akiwa kwenye daladala anajisifia kuwa na mtoto mwema, jamaa mwingine akaamua kumwuliza na mazungumuzo yao yalikuwa hivi,
Baba mtoto: Kwa kweli nina mtoto bommba sana, yaani nafurahia kuwa baba!
Jamaa: Anavuta sigara?
Baba mtoto: Hapana!
Jamaa: Anakunywa gongo?
Baba mtoto: Hapana!
Jamaa: Anarudi nyumbani usiku?
Baba mtoto: Hapana!
Jamaa: Kweli, nafikiri umepata mtoto mwema sana! Ana umri gani?
Baba mtoto: Juma tano ijayo atafikisha miezi sita!
**********



