Katika kile kinachoonekana ni kukosa umakini japo waswahili wanasema ‘ajali haina kinga’, jamaa mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja nchini India ambaye pia inasemekana alikuwa na tatizo la akili alipigwa na umeme na kufa papo hapo akiwa juu ya behewa la moja ya magari moshi ya nchini humo.
Aidha mhanga huyu inasadikika alipanda juu ya behewa na wasamalia wema walikuwa wanataka kumshusha kwani waliamini gari moshi hilo likianza kutembea litahatarisha maisha yake. Mwanzoni alionekana akibembelezwa na abiria waliokuwepo katika eneo hilo ili ateremke pasipo mafanikio.
Baada ya zoezi la kumshusha kutofanikiwa, marehemu alisimama akaanza kutembe juu ya behewa! Baada ya hatua kadhaa, marehemu alishika moja ya nyaya za umeme ambazo zilikuwa zinapita juu na kufariki dunia pale pale. Kitendo hicho kiliwashtua sana abiria waliokuwa wamepanda gari moshi hilo na baadhi ya watu waliokuwa karibu naye pale.
Hii Hapa Ni Video Ya Mkasa Huu Wa Kusikitisha

