Home Jamii Achomwa Vibaya | Kisa Ni Kiporo Cha Ugali!!!!!

Achomwa Vibaya | Kisa Ni Kiporo Cha Ugali!!!!!

558
0

Mtoto mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa, amechomwa vibaya sana na binamu yake kwa  maji ya moto baada ya kudaiwa kula kiporo cha ugali! Mkasa huo wa kusikitisha umetokea siku za hivi karibuni pale binti huyo alipoamka na kutoa vyombo mezani ili akavioshe. Mezani kulikuwa na bakuli la ugali na vyombo vingine vichafu. Binti huyo aliamua kukata ugali kidogo ili awalishe bata na kuku na mwingine akabakiza kwenye hilo bakuli.


Yule dada binamu alipoamka akamwuliza yule binti kama aliona ugali katika bakuli! Yule mtoto akasema ndio kauona, na yule dada akataka uletwe ule ugali na mazungumuzo yao yalikuwa hivi;

Dada: Mbona ugali upo kidogo?

Mtoto: Kiasi kidogo nimewapa bata.

Dada: Toka zako, acha uonngo umekula wewe!

Mtoto: Hapana nimewapa bata.

Dada: Twende nikaona ( Kwa bahati mbaya wale bata wakawa wamemaliza kuula ule ugali) Umekula mwenyewe halafu wawasingizia bata! Subiri nikuonyeshe!

mtoto1

Yule dada akachemsha maji kwenye birika na kumumwagia yule mtoto! Mtuhumiwa katoroka na anatafutwa na polisi ila mume wake anashikiliwa na polisi. Majirani wanasema kuwa binti huyo amekuwa akinyanyaswa sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here