Home Mbavu Zangu Jina lake lamponza stejini

Jina lake lamponza stejini

398
0

Msanii mmoja wa muziki wa kizazi kipya yaani bongo fleva anayefahamika kwa jina la KINYA alipata nafasi ya kuimba katika moja ya matamasha hapa nchini. Ni kawaida kila msanii anapokuwa jukwaani kujitambulisha kabla ya kuanza kutumbuiza. Kwa mfano utasikia wasanii wakijitambulisha ni Diamond hapa, ni Mez B hapa, ni Jay Dee hapa na kadhalika.

Msani huyu ilipofika zamu yake akaanza kwa kujitambulisha, “Yeah! Ni Kinya hapa…! X5” Mashabiki wakang’aka kwa sauti kubwa huku wakipiga makelele, “UTAZOAAAAA MWENYEWE”. Baadhi wakafika mbali zaidi, “Pumbavu kabisa, UTAKUNYAJE stejini, bwege mkubwa weee! Sisi tunataka MISTARI na sio MIMAVI YAKO!!!

**********