Home Vichekesho Nani Mjanja?

Nani Mjanja?

521
5

Mtanzania na Mkenya walienda super market kuangalia kama wanaweza kununua vitu. Baada ya kutoka Mkenya akawa anajigamba kwamba Wakenya ni wajanja sana kuliko Watanzania huku akimwonyesha Chokoleti tatu alizoziiba ndani ya super market.

Mtanzania akamshawishi Mkenya ili warudi tena ndani na yeye akamwonyeshe ujanja wake. Walipofika ndani Mtanzania akamwambia mhudumu;

Mtanzania: Nataka leo nikuonyeshe mazingaombwe

Mhudumu: Mazingaombwe gani hayo?

Mtanzania: Nipe Chokoleti tatu (Baada ya kupewa Yule Mtanzania akazila zote mbele ya mhudumu kisha akasema,) Unaona nimezila zote tatu lakini amini usiamini, chokoleti zako zote ziko mfukoni mwa huyu jamaa! (Anamwonyesha Mkenya)

Mhudumu akamkagua Mkenya na kweli akazikuta zile chokoleti tatu mfukoni mwake. Nani mjanja hapa?

**********


5 COMMENTS

Comments are closed.