Home Siasa Je, Huu Ndiyo Mwisho Wa Msigano Wa Wakubwa Hawa?

Je, Huu Ndiyo Mwisho Wa Msigano Wa Wakubwa Hawa?

837
2

Baada ya siku kama sio miezi kadhaa ya msigano wa kisiasa baina ya Rais J.M. Kikwete na P.Kagame hatimeye msigano huo unaweza ukawa umepata mwarobani. Marais hawa wamekutana mapema jana jijini Kampala kulikofanyika mkutano wa kujadili hali ya DRC inayoendelea hivi sasa.

JK NA KAGA

Kumekuwa na tuhuma za moja kwa moja zinazomshutumu Kagame kuwa sehemu ya mgogoro hivyo licha ya kukanusha mara kadhaa! Msigano uliibuka pale Rais Kikwete alipompa ushauri wa bure Rais Kagame ili amalize vita ya Congo kwani vidole vingi vimekuwa vikimnyoshea yeye kama mfadhili wa waasi M23!

Sakata hili lilionekana kuchukua sura mpya pale Rais Kikwete alipotangaza msako wa wahamiaji haramu waliopo nchini jambo ambalo wadadisi wa mambo wanadhani lilikusudia kuwatimua Wanyarwanda wengi ambao wamezagaa nchini bila kuwa na vibali halali vya kuishi Tanzania.

Naye Kagame alijibu mapigo pale inapodhaniwa kwa maelekezo yake alipandisha ushuru ghafla wa magari ya mizigo yanayoingia nchini Rwanda kutoka $ 152 mpaka $500.

JAKKK

Kumekuwa na mikakati ya makusudi kwa Rwanda kujitoa kutumia bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kupitishia mizigo yake jambo ambalo limeonyesha uhusiano mbaya baina ya nchi hizi.


Hata hivyo habari za hivi karibuni zinaeleza kuwa wakuu hawa wa nchi wamekubaliana kuendelea umoja na mshikamano kama uliokuwepo mwanzo. Hizi ni baadhi ya picha zilizopigwa jana katika mkutano huo.

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA.


2 COMMENTS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here