WIVU NI KIDONDA!!!
Jamaa mmoja mkazi wa Tabata amempa talaka tatu mkewe baada ya kukasirishwa na maneno yaliyokuwa yameandikwa kwenye khanga aliyovaa mkewe. Jamaa huyo alikuwa ni mtu wa safari nyingi sana kulingana na kazi zake!
Mara ya mwisho kabla ya sakata hilo kutokea, jamaa huyo alikua amesafiri kwa muda wa miezi mitatu, alishtuka aliporudi na kumkuta Mkewe amevaa khanga iliyoandikwa,
“HERI NIMPE JIRANI KULIKO KIOZEE NDANI”
Mume huyo mwenye wivu mkali alimjia juu mkewe kutaka aelezwe alikuwa na maana gani kuvaa khanga hiyo. Mkasaa huu ulitokea sebuleni tu mara baada ya kuingia nyumbani kwake.
Wakati mke anajaribu kujitetea jamaa akaona khanga nyingine iliyokuwa chumbani juu ya kitanda. Khanga hiyo ndiyo iliyofanya Talaka zitoke ilikua imeandikwa,
NIPE UTAMU”NITOE HAMU, MSAFIRI MWANA HARAMU”
Jee ungekua wewe ungefanya nini?



