Jamaa mmoja alienda juha alienda kumtembelea rafiki yake aliyekuwa anaumwa! Ukweli ni kwamba siku hizi maisha yamebana sana watu wala hawatembeleani. Alipofika kwa rafiki yake ambaye ameoa kwa bahati baya mvua ilianza kunyesha sana.
Yule mwenyeji akamshawishi rafiki yake alale kwake kwani mvua ilikuwa kubwa sana, kwa kuwa mwenyeji alikuwa na chumba kimoja alimwomba rafiki yake alale sebuleni. Jamaa akakubali na akasema atalala.
Ukafika wakati wa kulala yule mwenyeji akaingia chumbani na mkewe akimwacha rafiki yake sebuleni. Baada ya saa mbili, yule mwenyeji akatoka nje kwenda kujisaidia na alipofika sebuleni akamwona rafiki yake ameloa chepechepe huku anatetemeka kwa baridi kali.
Ikabidi yule mwenyeji amwulize rafiki yake;
Mwenyeji: Ndugu, mbona hivyo????
Jamaa: Nilienda nyumbani kuchukua shuka!
**********




