Home Vichekesho Usithubutu Kupuuza Ujumbe Wowote!!

Usithubutu Kupuuza Ujumbe Wowote!!

388
0

Unajua tabia ya kupuuza ujumbe ni mbaya sana. Siku moja jamaa mmoja alikuwa mahututi na akawa amelazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum yaani ICU. Ndugu wa mgonjwa walipoona hali ya ndugu yao ni mbaya waliamua kwenda kumtafuta Mchungaji aje amwombee mgonjwa!

Mchungaji akiwa anaendelea na maombi, ghafla mgonjwa akanyanyuka na kuchukua kalamu na karatasi vilivyokuwa kwenye meza pembeni ya kitanda chake na kuandika kitu kisha akampa mchungaji. Mchungaji alipokea kile kikaratasi akakiweka mfukoni akaendelea na maombi. Akiwa anaendelea kuomba ghafla Yule mgonjwa akakata roho!

Baada ya mazishi na taratibu nyingine kufanywa, mchungaji aliwaambia ndugu wa marehemu kwamba kuna ujumbe ambao alipewa na marehemu kabla hajafa! Bila kuisoma mchungaaji akampa ndugu wa marehemu ausome! Karatasi ilikuwa imeandikwa hivi;

“Pasta umekanyaga mpira wa Oksijeni,nakosa hewa.”

Kwa hasira ndugu wa marehemu wakamzika mchungaji mzima mzima!