Home Vichekesho Usipende Kutongoza ovyo, Itakula Kwako Siku Moja!

Usipende Kutongoza ovyo, Itakula Kwako Siku Moja!

713
1

Kunyoa-saluni

Jamaa mmoja ambaye aliacha kazi iliyompeleka saluni ya kunyoa nywele zake na kujikuta kaanzisha biashara nyingine. Ni kawaida kwa sasa ukiingia saluni za kisasa za kiume kuona wanawake ambao husafisha nyuso za wateja wao na kuwaosha nywele pindi wanapomaliza kunyolewa.


Huyo jamaa alienda kwa lengo la kunyolewa na wakati ananyolewa macho yake yakakutana ana kwa ana na macho ya mrembo mmoja aliyekuwa ameshika taulo na jamaa huyo bila hiyana akaanzisha mazungumuzo:

Jamaa: Mrembo, umeumbika sana! Tunaweza toka ‘out’ baada ya kazi?

Mrembo: Hapana, nimeolewa mie!

Jamaa: Mwambie mumeo umeenda hospitali kumwangalia rafiki yako mgonjwa.

Mrembo: Mwambie mwenyewe, ni huyo anayekunyoa!

Ghafla jamaa akapooza ikabidi aage anaenda kujisaidia chooni na hakurudi tena huku akiwa kanyolewa upande.

**********


1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here