Home Vichekesho Ulevi Kipaji; Chezea ‘Machozi Ya Simba’ Wewe!!!!

Ulevi Kipaji; Chezea ‘Machozi Ya Simba’ Wewe!!!!

374
1

Walevi wawili walikuwa ni wateja wakubwa sana wa mama Chichi, mwanamama hodari wa kupika machozi ya simba yakapikika yaani gongo katika mitaa fulani hivi hapa Daslam!

Siku moja walevi hao walikausha pombe mapema kama milango ya saa 11 jioni hivyo wakaamua kujisogeza majumbani kwao. Kwa bahati nzuri walikuwa ni majirani hivyo njia ilikuwa ni moja ya kurudia nyumbani. Wakiwa njiani mlevi aliyekuwa ametangulia akaona kitu kinang’aa sana chini akakiokota kumbe kilikuwa ni kioo! Alipokitazama macho yakamtoka sana kisha akamwambia mwenzake,


Mlevi wa kwanza: Hii sura si ngeni machoni mwangu sema jina tu silikumbuki!

Mlevi wa pili: Hebu nione! (akapewa kioo) Wee bwege kweli tena huna akili, si mimi huyu? Halafu unajidai hunikumbuki, nyie ndio mkiwini maisha mnatutosa masela wenu wa kitambo! Ushanikera kesho sikununulii pombe!

Wakaachana kila mmoja akapita njia yake baada ya hali ya hewa kuchafuka!

**********

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here