Home Vichekesho Ukitenda Dhambi Jehanamu Ni Yako Tu!

Ukitenda Dhambi Jehanamu Ni Yako Tu!

535
0

Pombe ni mbaya na ulevi ni noma, mlevi mmoja alipita katika viwanja fulani akakuta kuna mahubiri ya neno la Mungu. Mtumishi wa Bwana alikuwa anawafundisha kondoo wake wasitende dhambi na wamgeukie Mungu maana hakika kiama ya wafu ipo na Jehanamu ipo pia.

Alichagiza kwa kuzitaja dhambi zote ambazo Mungu amewakataza watu wake wasizifanye. Wakati anazitaja ilifika wakati wa kukemea walevi na wanywa pombe;


Mchungaji: Ole wenu mtendao dhambi sasa mtakutana na moto mkubwa sana siku ya kiama. Ole wenu nyie wazinzi, waasherati, wezi, waongo, wauaji na walevi wa pombe za aina zote!

Baada ya kutaja kipengele cha pombe yule mlevi akaropoka kwa sauti kubwa;

Mlevi: Nyie mtendao mema ole wenu mkifika huko peponi mkipewa mahindi mabichi msije kutuomba moto wetu,tutawatoa nishai mbele ya Sir God labda mwende na mkaa wenu!

**********





LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here