Home Vichekesho Sema Tu Unataka Maji, Mimi Zeruzeru! | Chezea Kizungu Weye!

Sema Tu Unataka Maji, Mimi Zeruzeru! | Chezea Kizungu Weye!

351
0

zeruzeru-tu

Wabongo tuna tabia moja chafu sana ya kuwagwaya Wazungu. Yaani ni kawaida sana kwa mbongo kumshobokea mzungu  kuliko mbongo mwenzake. Jamaa mmoja alikuwa anafanya kazi posta mpya Daslam. Si unajua tena kule sio wote wanaofanya kazi ni matawi ya juu hivyo huwa wanapata shida sana kujilinganisha na wenye uwezo wao.


Lakini wapo wadau ambao huwa hawavungi, wanafanya kazi ghorofa ya 5 kwenye jengo la Benjamini Mkapa ila wanakula mihogo na Mountain Dew mitaa fulani ya posta na maisha yanaendelea. Jamaa huyo alikuwa ni mmoja wa wadau wanakula mihogo ya kukaanga kila siku na soda ili kukwepa gharama za vyakula vya posta.

Siku moja akiwa anakula majira ya mchana kwa bahati mbaya kipande cha mhogo kikamkwama na pembeni yake kulikuwa na mzungu ana maji ya kunywa huku naye anakula mihogo. Jamaa ikabidi aanze,

Jamaa: Ze zee Cassava is standing at ze koromero, pliz water!

Mzungu: Utakufa mdogo wangu, sema unaomba maji mimi ni zeruzeru tu!

**********



LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here