Home Vichekesho Pombe Na Mbingu

Pombe Na Mbingu

441
0

Mchaga mmoja cha pombe alipanda kipanya (hiace) ili impeleke alikokuwa anaelekea katika shughuli zake za ulevi ambazo kwake ni kawaida kuifata pombe pahala popote ili mradi iwe ni pombe ya bure. Akiwa katika hiece, mlevi huyo alianza kuongea na konda wa daladala hilo na mazungumuzo yao yalikuwa hivi,


Konda: Duh! Hii tabia yako ya ulevi hutafika mbinguni!

Mlevi: Yesu na Maria! Nishushe hapa hapa, kumbe mnaenda mbinguni. Mimi siendi mbinguni, naenda zangu Marangu mtoni kupitia Kilema na kuingia Kirua kuna MBEGE kwa ndugu yangu! Ubarikiwe konda kwa kuropoka leo ningekosa uhondo, nishushe nipande ya Marangu!

**********

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here