Home Vichekesho Mweeeee! Nyama Ya Kuku!

Mweeeee! Nyama Ya Kuku!

742
1

Wanawake-wa-Mjini

Unajua maisha ya mjini yana vituko sana hasa hapa Daslaam. Watu wamekuwa wakiishi maisha ya ajabu kuyasimulia na kwa kweli yanatia simanzi. Mama mmoja wa mitaa fulani ya uswazi huko Kinondoni alikuwa anabadilishana mawazo na jirani yake.

Mwanamke wa kwanza: Shoga yangu nina hamu na nyama ya kuku!

Mwanamke wa pili: Kuku????

Mwanamke wa kwanza: Ndiyo!!!


Mwanamke wa pili: Hongera walio shamba ambao wakichinja kuku wanamla hapo hapo lakini sio Dar! Hapa Dar kuku anachinjwa Kitunda, Shingo inaliwa Kinondoni, Kibawa kinaliwa Manzese, Kidali chaliwa Tabata, Paja Osterbay, Firigisi Masaki, Miguu Mbagala, Mbavu Mikocheni, Utumbo Tandika, Kichwa Tandale kwa Mtogole, Mgongo Mwenge, Ngozi Keko! Nyama ya kuku  kwetu kama mgao wa UMEME, kila mtu lazima apate! Haya Shoga, umesema una hamu ya kula kuu au Shingo ya kuku?

Mwanamke wa kwanza: Shoga, hata hamu imeniisha!

**********


1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here