Home Mbavu Zangu Mtu Chake Bwana!

Mtu Chake Bwana!

789
0

Jamaa mmoja kwa kupenda misifa alikuwa anawaiba sana wake za watu! Kwa bahati mbaya siku moja akafumaniwa na mwenye mke kwa hasira akamroga jamaa nyeti zake zikapotea akawa flati. Kwa kuwa jamaa alikuwa na mke ikabidi amdanganye anaumwa ili mkewe asimshtukie.

Rafiki yake akamshauri aende akamwombe msamaha mwenye mke ili arudishiwe nyeti zake. Bila hiyana yule bwana mwenye mke akamsamehe jamaa na akaletewa ungo wenye nyeti nyingi akamwambia achague ya kwake. Baada ya kuhangaika sana akashindwa kuitambua ikabidi aende kwa mkewe kuungama kosa lake ili akamsaidie kuitambua nyeti yake.

Ile kufika tu mke wake akaangali kisha akasema,

Mke: Hii kubwa ni ya Patrick yule fundi viatu, hii nyeupe nia yule mpemba mwenye duka la ‘ice cream’, hii nyembamba ni ya jirani yetu Muna, ya kwetu hii hapa inafanana sana na ya mjeshi mpangaji wa chumba cha pili.

Je, ingekuwa wewe ndio mume ungefanyaje?

**********