Hakika nina amini kila mtu amewahi kuguswa na machungu ya kifo cha mtu wake wa karibu sana. Hii ina maana kila mtu anafahamu maumivu ya kufiwa na mtu ambaye unampenda.
Jamaa mmoja alifiwa na mkewe kipenzi jambo lililomjaza huzuni kubwa sana wakati wote. Alikuwa akilia sana kila mara anapokumbuka sura nzuri ya mke wake na tabia zake njema.
Kuna vitu vingi sana vilikuwa vinarudisha kumbukumbu za mkewe vikiwemo picha, nguo na vinginevyo. Kila alipokuwa akipekuwa nguo na vitu vingine vya marehemu vilimwongezea uchungu sana. Ghafla jamaa akaziona nguo za ndani za mkewe yaani chupi, kitendo kile kilimfanya aangue kilio kikubwa sana huku akighalaghala.
Majirani na marafiki wakampoza pale huku wakimbembeleza na kumhoji taratibu kwa nini analia sana;
Jirani: Kulikoni, mbona walia sana na kilio kimeongezeka ghafla ulipoziona nguo za ndani za mkeo?
Jamaa: Nina uchungu x5 Sanaaaaaaaaaaaaaaaaaa! (Huku akimwonyesha ile chupi jirani yake ) Nakumbuka kilichokuwepo humu, sitakipata tena!
**********




