Siku moja mwanaume mmoja alifika kwake akiwa anahema akitokea kazini kabla ya muda wa kawaida. Akamwambia mke wake,
Mume: Jiandae haraka tuna safiri kwenda mbeya
Mke: Kuna nini??
Mume: Mama amefariki!
Mke: Mimi siwezi kwenda kilioni nikiwa hivi!
Basi mke akaenda saluni akaweka nywele vizuri na kubandika kope za macho. Aliporudi akaanza kupanga nguo,akamuuliza mumewe,
Mke: Huvo mama yako amefariki kwa nini?
Mume: Mama yangu hana kitu, nimetoka kuongea naye sasa hivi.
Mke: Si umeniambia kuwa kuna msiba?
Mume: Ndiyo, mama yako kafariki!
Ghafla mkewe akaanza kughalaghala na kupiga kelele,
Mke: Niwahishe haraka nyumbani nikamzike mama nisije kuta wamezika!
Mume: Siwezi kwenda msibani nikiwa hivi, subiri nikanyoe ndevu.
Ama kweli mkuki kwa nguruwe…!!!




